Margaret Mensah-Williams

Margaret Mensah-Williams

Mensah-Williams mwaka 2017
Amezaliwa 1961
Mariental, Namibia
Nchi Namibia
Kazi yake Mwanasiasa


Margaret Natalie Mensah-Williams (amezaliwa tarehe 25 Desemba 1961) ni mwanasiasa, mwanadiplomasia na mwanachama mashuhuri wa SWAPO nchini Namibia. Anahudumu kama balozi wa Namibia nchini Marekani hadi sasa [1] .

Mensah-Williams pia alihudumu kama mjumbe wa baraza la Windhoek katika jimbo la Khomasdal Kaskazini kuanzia mwaka 1998 hadi 2019, na kutoka katika nafasi hii alichaguliwa kuwakilisha Mkoa wa Khomas katika Baraza la Kitaifa la Namibia, chombo cha juu cha Bunge la Namibia kuanzia mwaka 2015 hadi 2019. Katika Baraza la Kitaifa, alichaguliwa kuwa naibu mwenyekiti mwaka 1998, na Orodha ya wenyeviti wa Baraza la Kitaifa la Namibia mwaka 2015. Alichukua uamuzi wa kujiuzulu kutoka kwenye nyadhifa zote za uwakilishi wa kikanda kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Namibia mwaka 2019 ili kugombea kiti katika Bunge la Kitaifa (Namibia), chombo cha chini cha Bunge la Namibia, na baadaye akawa mbunge[2].

  1. https://namibiaembassyusa.org/about-embassy/
  2. https://www.gsws.ae/speaker/ms-margaret-mensah-williams/

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search